Hii hapa orodha ya majina ya walioitwa kwenye usaili Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida anapenda kuwataarifu waombaji kazi za kujitolea zilizotangazwa tarehe 28/04/2026 kuwa usaili unatarajiwa kufanyika tarehe 22/05/2026 saa 02:00 asubuhi. Usaili utafanyika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida kwenye Ukumbi wa Mikutano (Morning Meeting).
Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wanatakiwa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-
- Kufika na vyeti halisi vya Elimu na Taaluma (Original Certificates).
- Cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate).
- Watakaowasilisha hati ya matokeo (Result Slip) au Transcript bila cheti halisi hawatakubaliwa kufanya usaili.
- Leseni halisi kwa kada zenye leseni.
- Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au Kitambulisho cha Mpiga Kura.
Zingatia:
Wasailiwa wote wanatakiwa kufika eneo la usaili kwa muda uliotajwa.
Leave a Reply
View Comments