Home Ajira Kuitwa kwenye Usaili TRA 2025 PDF na Ratiba
Ajira

Kuitwa kwenye Usaili TRA 2025 PDF na Ratiba

Kuitwa kwenye Usaili TRA 2025 PDF na Ratiba
Kuitwa kwenye Usaili TRA 2025 PDF na Ratiba

Hii hapa orodha ya majina ya walioitwa au kuitwa kwenye usaili TRA 2025 na ratiba katika PDF Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwataarifu wasailiwa wote waliofaulu mtihani wa mchujo na kuchaguliwa (SELECTED) kuwa usaili wa vitendo na mahojiano (Practical and Oral Interviews) utafanyika kuanzia tarehe 02 Mei, 2025 hadi tarehe 14 Mei, 2025.
Waombaji watakaofaulu usaili huo wataajiriwa rasmi.

Wasailiwa wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:

1. Kitambulisho cha Utambulisho

Kila msailiwa anatakiwa kuja na kitambulisho halali kwa ajili ya utambuzi. Vitambulisho vinavyokubalika ni:

  • Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
  • Kitambulisho cha Mkazi
  • Kitambulisho cha Mpiga Kura
  • Leseni ya Udereva
  • Hati ya Kusafiria
  • Barua ya Utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa

Pakua PDF hapa ya ratiba ya usaili TRA

Vitambulisho tofauti na hivyo havitatambuliwa. Pia, Matokeo ya usaili wa mahojiano na kuandika yatawekwa hapa.

2. Vyeti vya Kielimu

Msailiwa anatakiwa kufika na vyeti halisi (original) vifuatavyo, kulingana na sifa za nafasi aliyotuma:

  • Cheti cha Kuzaliwa
  • Cheti cha Kidato cha IV
  • Cheti cha Kidato cha VI
  • Diploma (Stashahada)
  • Higher Diploma
  • Shahada au vyeti vya juu zaidi

HAZITAKUBALIWA:

  • Testimonials
  • Provisional Results
  • Statement of Results
  • Form IV na VI Result Slips

Wasailiwa watakaowasilisha vyeti hivyo hawataruhusiwa kuendelea na usaili.

Pakua PDF hapa ya majina walioitwa kwenye usaili TRA

3. Gharama za Usaili

TRA haitagharamia chochote. Kila msailiwa anapaswa kujigharamia kwa:

  • Chakula
  • Usafiri
  • Malazi

4. Ratiba na Mahali pa Usaili

  • Wasailiwa wanapaswa kufika kulingana na tarehe na eneo walilopangiwa kwa mujibu wa ratiba.
  • Muda wa kufika ni saa 1:00 kamili asubuhi.

5. Vyeti vya Waliosoma Nje ya Nchi

Wasailiwa waliosoma nje ya Tanzania wanatakiwa kuhakikisha vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika kama:

  • TCU
  • NACTVET
  • NECTA

6. Vyeti vya Usajili kwa Kada Maalum

Kwa kada zinazohitaji usajili wa kitaaluma, wasailiwa wanapaswa kuja na:

  • Vyeti vya usajili
  • Leseni halali za kufanya kazi

7. Vifaa Visivyoruhusiwa

Msailiwa haruhusiwi kuingia kwenye eneo la usaili akiwa na:

  • Simu ya mkononi
  • Saa
  • Kifaa chochote cha kielektroniki

8. Mawasiliano kwa Maelezo Zaidi

Kwa taarifa au ufafanuzi zaidi, tembelea ofisi ya TRA iliyo karibu nawe au wasiliana kupitia:
Tovuti: www.tra.go.tz
Simu bila malipo: 0800 780078 / 0800 750075
WhatsApp: 0744 23 33 33
Barua pepe: huduma@tra.go.tz / services@tra.go.tz

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Newala 2025
Ajira

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Newala 2025

Haya hapa matokeo ya ajira na majina ya Walioitwa kwenye Usaili Newala...

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Manispaa ya Temeke 2025
Ajira

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Manispaa ya Temeke 2025

Haya hapa matokeo ya ajira na majina ya Walioitwa kwenye Usaili Temeke...

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Buhigwe 2025
Ajira

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Buhigwe 2025

Haya hapa matokeo ya ajira na majina ya Walioitwa kwenye Usaili Buhigwe...

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Malinyi 2025
Ajira

Matokeo ya Ajira Walioitwa kwenye Usaili Malinyi 2025

Haya hapa matokeo ya ajira na majina ya Walioitwa kwenye Usaili Malinyi...